Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake
Idara ya Wanawake imeanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 20 sehemu ya 7 ya katiba ya Tanzania Assemblies of God. Hivyo kutokana na msingi huo Idara ya WWK imeandaa taratibu na muongozo wa Idara ya WWK kwa msingi wa kuongoza na kusimamia shughuli zote za Idara hii.
Kuwa na wanawake wa kanisa la TAG mbao ni jeshi halisi la Bwana Yesu, walio jaa nguvu za roho mtakatifu, wenye kasi yakueneza na kutegemeza injili ambao maisha yao na ya jamii inayowazunguka huwa bora kwa mjibu wa kanuni za kibiblia. Pia idara ya WWK ipo kwaajili ya kuwaunganisha wanawake wote wa kanisa la TAG kitaifa na kanisa la mahali pamoja kwa kuwakuza kiroho, kuwapandikiza maono na mzigo wa kutumika na kutoa mafundisho yatakayowawezesha wanawake katika kanisa ili kutimiza agizo kuu kwa kutenda na kutoa mali zao
Wanawake wanaotangaza Injili ni jeshi kubwa
Idara ya WWK ni moja kati ya idara za kanisa la Tanzania Assemblies of God inayohusika na kupanga na kusimamia shughuli za kimkakati za wanawake katika ngazi zote za kanisa. soma zaidi
Mnamo mwaka 2008, Mchungaji Dr. Barnabas Mtokambali alichaguliwa kuwa askofu mkuu wa awamu ya tatu ya kanisa la Tanzania Assemblies of God. Ndipo Mrs. Faraja Hamuli akateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa WWK. Pamoja naye, ilikuwepo kamati ya utendaji ambayo wajumbe wake walikuwa ni Mrs. Eshimendi Swai (Makamu mkurugenzi Mkuu), Mrs. Josephine Manda (Katibu Mkuu), Mrs. Neema seng'enge (Mtunza hazina Mkuu) na Mrs. Gladmary Mtokambali (mshauri Mkuu).
Idara ya WWK ni maalum kwaajili ya wanawake wote wa Tanzania Assemblies of God.
Tushirikiane pamoja katika kutekeleza mpango mkakati sisi kama Wanawake kwani kwa umoja na pamoja tutatenda makuu.
MKURUGENZI MKUU
MAKAMU MKURUGENZI MKUU
KATIBU MKUU
MHAZINI MKUU
Wanawake watumishi wa Kristo.
Hii ndio kamati kuu tendaji kitaifa katika idara ya WWK.
Askofu mkuu wa TAG mnamo tarehe 28 mwezi wa pili aliapishwa Rasmi na kua Mwenyekiti wa CPCT.
Semina za ILI zinatarajiwa kuanza hivi karibuni hivyo basi viongozi na wanachama wote wanaotakiwa kuhudhulia msipange kukosa.
Kwenye semina za uongozi za ili kutakua na Mafunzo pia kuhusu Mfumo wetu wa Bezaleli hivyo basi Kamati za Sehemu, Kamati za Idara Sehemu na Jimbo mnahimizwa kuhudhulia.
soma zaidiKutakua na Semina ya Uongozi ya ILI zitakazofanyika CCT, Morogoro hivyo basi Waalimu wa Vyuo Mama na Wenza Wao wanahimizwa kufika bila kukosa.
soma zaidiKutakua na kikao cha tathmini ya robo ya I ya mwaka kitakachofanyika Morogoro na wahusika wakuu ni Kamati ya Utendaji /Menejimenti
soma zaidi