Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake






Wanawake Watumishi wa wamchao wampendao Kristo

Idara ya Wanawake imeanzishwa kwa mujibu wa ibara ya 20 sehemu ya 7 ya katiba ya Tanzania Assemblies of God. Hivyo kutokana na msingi huo Idara ya WWK imeandaa taratibu na muongozo wa Idara ya WWK kwa msingi wa kuongoza na kusimamia shughuli zote za Idara hii.

Dhima Yetu

Kuwa na wanawake wa kanisa la TAG mbao ni jeshi halisi la Bwana Yesu, walio jaa nguvu za roho mtakatifu, wenye kasi yakueneza na kutegemeza injili ambao maisha yao na ya jamii inayowazunguka huwa bora kwa mjibu wa kanuni za kibiblia. Pia idara ya WWK ipo kwaajili ya kuwaunganisha wanawake wote wa kanisa la TAG kitaifa na kanisa la mahali pamoja kwa kuwakuza kiroho, kuwapandikiza maono na mzigo wa kutumika na kutoa mafundisho yatakayowawezesha wanawake katika kanisa ili kutimiza agizo kuu kwa kutenda na kutoa mali zao

Maadili yetu

  1. Uaminifu kwa Biblia kwa kuishi mafundisho yake.
  2. Kuwajibika kijamii tukidhihirisha upendo na Haki ya Mungu katika maneno na matendo.
  3. Kufanya pamoja kama timu kwa kua na mahusiaono mema baina yetu na watu wengine.
  4. Kuvuna Kimkakati.
  5. Kuwawezesha viongozi.
  6. Kukua kimkakati.
  7. Utawala wa fedha unaowajibika.

Makusudi yetu

  1. Kuiletea Nyumba baraka kwa kua mke bora katika familia
  2. Kuliletea kanisa baraka kwa kushiriki huduma zote zinazohusu kanisa la mahali pamoja na kutoa fungu la kumi na michango yote ya kanisa kwa Uaminifu.
  3. Kumletea mchungaji na familia yake baraka kwa kumuombea mchungaji na familia yake pamoja na kuwasaidia katika mahitaji mengine.
  4. Kukiletea kijiji/mtaa baraka kwa kushiriki huduma zute za kijamii na kuonesha upendo wa kweli kimaneno na matendo.

Sisi ni Nani nani?

Wanawake wanaotangaza Injili ni jeshi kubwa

Idara ya WWK ni moja kati ya idara za kanisa la Tanzania Assemblies of God inayohusika na kupanga na kusimamia shughuli za kimkakati za wanawake katika ngazi zote za kanisa. soma zaidi

Kuhusu Uongozi

Mnamo mwaka 2008, Mchungaji Dr. Barnabas Mtokambali alichaguliwa kuwa askofu mkuu wa awamu ya tatu ya kanisa la Tanzania Assemblies of God. Ndipo Mrs. Faraja Hamuli akateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa WWK. Pamoja naye, ilikuwepo kamati ya utendaji ambayo wajumbe wake walikuwa ni Mrs. Eshimendi Swai (Makamu mkurugenzi Mkuu), Mrs. Josephine Manda (Katibu Mkuu), Mrs. Neema seng'enge (Mtunza hazina Mkuu) na Mrs. Gladmary Mtokambali (mshauri Mkuu).

kamati kuu ya Idara kitaifa

Wanawake watumishi wa Kristo.

Hii ndio kamati kuu tendaji kitaifa katika idara ya WWK.

Habari za Hivi Karibuni

SEMINA ZA ILI

Semina za ILI zinatarajiwa kuanza hivi karibuni hivyo basi viongozi na wanachama wote wanaotakiwa kuhudhulia msipange kukosa.

Limetolewa na Ofisi Kuu

Matukio ya Hivi karibuni kwa mwezi huu

Mafunzo ya Bezaleli

Kwenye semina za uongozi za ili kutakua na Mafunzo pia kuhusu Mfumo wetu wa Bezaleli hivyo basi Kamati za Sehemu, Kamati za Idara Sehemu na Jimbo mnahimizwa kuhudhulia.

soma zaidi
27 - 31 Ma

Semina ya Uongozi ya ILI

Kutakua na Semina ya Uongozi ya ILI zitakazofanyika CCT, Morogoro hivyo basi Waalimu wa Vyuo Mama na Wenza Wao wanahimizwa kufika bila kukosa.

soma zaidi