TUMAINI PENSION FUND

Kuhusu TPF
Mfuko wa Mafao wa Tumaini (TPF) ulianzishwa 01/01/2019 na kanisa la TAG ili kutoa huduma za hifadhi ya jamii kwa watumushi wake.
Maono
Kuwa Mfuko wa mafao wa mfano kwa mifuko mingine ya ziada nchini
Maadili
Uwazi, Uaminifu, Uadilifu, Uwajibikaji, Ubunifu, Kufanya kazi kwa kushirikiana na Huduma kwa wakati
Dhima
Kutoa huduma bora ya hifadhi ya jamii kwa watumishi kwa kuzingatia misingi ya imani ya kanisa
Mafao ya Uzeeni
Kusudi la msingi la pensheni ya uzee ni kumhakikishia usalama wa kipato mtumishi aliyeishiwa nguvu kwa sababu ya uzee. Mtumishi anapokea kipato kila mwezi.
Mafao ya Urithi
Pensheni ya urithi inalipwa kwa wategemezi wa mtumishi mwanachama wa TPF aliyepoteza uhai. Mafao ya urithi yamekusudiwa kufidia upotevu wa msaada wa kiuchumi uliokuwa ukitolewa na mtumishi aliyepoteza uhai.
Mafao ya Ulemavu
Pensheni ya ulemavu inalipwa kwa mtumishi aliyepoteza uwezo wa kufanya kazi kwa sababu ya ulemavu wa kudumu uliosababishwa na ajali au ugonjwa
Mfuko wa Mafao wa Tumaini (TPF) upo kwa ajili ya kukuhudumia wewe Mchungaji wa kanisa la Tanzania Assemblies of God