Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake






Kuhusu Idara ya Uinjilisti
Huduma ya Uinjilisti ilianza rasmi Mwaka 1940 kupitia Wazee wetu (Wainjilisti watano); Rev Emmanuel Lazaro, Rev Moses Kulola, Rev Christian Kiwia, Ev Mathias Ng’andu na Rev Daudi Kuselya. Hawa walikuwa Wainjilisti wa mwanzoni kabisa ambao walihubiri kila kona ya Tanzania na kuhakikisha wanapanda makanisa ...Mwaka 2004, Idara ya Uinjilisti ilianzishwa rasmi katika kanisa la TAG, baada ya pendekezo la kuanzishwa kwake na kupitishwa na Halmashauri Kuu. Pamoja na mikutano Mikubwa ya Injili iliyofanyika huko nyuma, bado hapakuwa na chombo rasmi kitaifa cha kuratibu huduma hizi za Uinjilisti isipokuwa kulikuwa na Kamati tu zilizoundwa kwa kusudi husika la kuandaa mikutano hiyo mpaka mwaka 2004 ambapo Idara ya Uinjilisti Kitaifa ilipoanzishwa rasmi.
Bofya hapa kutembelea tovuti yetu

layout styles

DHIMA

Ni kuhakikisha Injili inahubiriwa kwa nguvu za Roho Mtakatifu, Kwa njia inayoendana na mazingira ili watu wa Tanzania na ulimwenguni kote wapate kusikia habari za Bwana na Mwokozi Yesu Kristo kwa lengo la kuwafanya wawe Wanafunzi wake.

KUSUDI

  • Kuhamasisha na kueneza huduma za Uinjilisti kitaifa.
  • Kuleta Uamsho na kutunza utakatifu ili moto wa Uamsho usizimike.
  • Kuibua na kuibua vipawa vya uinjilisti wa ngazi mbalimbali.

MAADILI

  • Uaminifu kwa Biblia.
  • Uadilifu.
  • Wajibu kwa jamii kwa kuonesha taswira ya upendo na haki kwa watu wote.
  • Kuvuna kwa pamoja.
  • Kuvuna Kimkakati.

VIONGOZI WA IDARA KITAIFA

Habari za Hivi Karibuni

SEMINA ZA ILI

Semina za ILI zinatarajiwa kuanza hivi karibuni hivyo basi viongozi na wanachama wote wanaotakiwa kuhudhulia msipange kukosa.

Limetolewa na Ofisi Kuu

Matukio ya Hivi karibuni kwa mwezi huu

Mafunzo ya Bezaleli

Kwenye semina za uongozi za ili kutakua na Mafunzo pia kuhusu Mfumo wetu wa Bezaleli hivyo basi Kamati za Sehemu, Kamati za Idara Sehemu na Jimbo mnahimizwa kuhudhulia.

soma zaidi
27 - 31 Ma

Semina ya Uongozi ya ILI

Kutakua na Semina ya Uongozi ya ILI zitakazofanyika CCT, Morogoro hivyo basi Waalimu wa Vyuo Mama na Wenza Wao wanahimizwa kufika bila kukosa.

soma zaidi