Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake
Idara hii ilizaliwa rasmi mwaka 2008 na ikakabidhiwa kama ofisi rasmi na Mchungaji David mwakajinga tarehe 12/12/2008. Jambo hili lilikuwa ni utekelezaji wa matakwa ya katiba ya Tanzania Assemblies of God iliyokuwa imeagiza kuwepo na Idara hii. Vile vile Idara hii ilianzishwa kama chombo cha utekelezaji wa mpango mkakati wa kwanza wa kanisa chini ya Askofu mkuu mpya na wa awamu ya tatu ya maaskofu watanzania, Dktr, Barnabas Mtokambali. Viongozi waanzilishi walikua ni Rev. Elingarami Munisi aliyekua Mkurugenzi Mkuu, Rev, profesa Joseph Kimeme aliyekua Makamu wake, Rev. Moses Magembe aliyekuwa Katibu Mkuu wa Idara na huu ndio ukawa mwanzo wa Idara hii. Bofya hapa kutembelea tovuti yetu
Kuwa Idara inayofanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo kitaifa na Kiulimwengu, waliojazwa na Roho Mtakatifu na wenye ushirika wa kiroho, Kufanya huduma inayoendana na mazingira na hivyo kulizidisha kanisa.
Kama Mkono wa TAG wa kutekeleza mpango mkakati, Idara hii itatimiza dira yake kwa kumjengea mshirika wa TAG msingi wa kuona maana ya kibiblia ya kumwabudu MUNGU. Pia ili mshirika aweze kukua kiibada, kihuduma, kiushirika na wenzake na kiutoaji chini ya uongozi na nguvu za Roho Mtakatifu.
|
Askofu mkuu wa TAG mnamo tarehe 28 mwezi wa pili aliapishwa Rasmi na kua Mwenyekiti wa CPCT.
Semina za ILI zinatarajiwa kuanza hivi karibuni hivyo basi viongozi na wanachama wote wanaotakiwa kuhudhulia msipange kukosa.
Kwenye semina za uongozi za ili kutakua na Mafunzo pia kuhusu Mfumo wetu wa Bezaleli hivyo basi Kamati za Sehemu, Kamati za Idara Sehemu na Jimbo mnahimizwa kuhudhulia.
soma zaidiKutakua na Semina ya Uongozi ya ILI zitakazofanyika CCT, Morogoro hivyo basi Waalimu wa Vyuo Mama na Wenza Wao wanahimizwa kufika bila kukosa.
soma zaidiKutakua na kikao cha tathmini ya robo ya I ya mwaka kitakachofanyika Morogoro na wahusika wakuu ni Kamati ya Utendaji /Menejimenti
soma zaidi