Wanaume taifa kubwa la Watendakazi wa Wamchao Kristo.
Kuwepo kwa Idara hii kunahamasisha wanaushirika huu kufanya uamuzi wa dhati kuleta mabadiliko katika maisha yao na jamii yote.
Kuhusu Sisi

Maono ya CMF ni kuona mwanamume aliyerejea katika nafasi yake ya awali ya uumbaji wa Mungu na kufanyika sifa na utukufu wa Kristo ili kutimiza kusudi la Kristo kupitia Kanisa pamoja na malengo ya TAG kitaifa.
Kuwajenga na kuwaunganisha wanaume ambao ni washirika wa TAG ili kukuza umoja na ushirika miongoni mwao na kati yao na Kanisa (Mdo 2:44-47), Kujifunza kanuni mbalimbali za ki-Mungu za kufanikiwa kiroho na kimaisha ili kuwa kielelezo kizuri katika familia na jamii.
CMF ipo ili kuwezesha wanaume kuabudu, kuwa na ushirika, kujengana, kutumika na kufanya uinjilisti.