Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake
CASFETA ni jumuiya ya wanafunzi walio mabalozi wa Kristo Tanzania yenye malengo tangu kuanzishwa kwake. Ushirika huu ni hitaji la wanafunzi walioko shule za sekondari na vyuoni kumuabudu Mungu kulingana na imani ya Kipentekoste. CASFETA ilianzishwa mwaka 1992. Wazo lake lilianzia kwa viongozi wa Idara ya vijana wa TAG, yaani Christ’s Ambassadors (CAs). Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CAs, mchungaji Uswege Mwakisyala alikuwa ndiye Mwenyekiti wa kamati ya watu watatu. Askofu Mkuu wa wakati huo Mchungaji Ranwel Mwenisongole alijibu kwa barua yake ya tarehe 8/10/1992, kuikubali huduma hiyo ianzishwe na kusimamiwa na idara ya Vijana CAs. CASFETA ilipata Mkurugenzi mpya 2008, Mch. Dkt. Huruma Nkone ambaye katika uongozi wake iliendelea kukua na kuzifikia shule, vyuo na vyuo vikuu vingi hapa nchini Tanzania, ambapo hadi kufikia mwaka 2020 kumekuwa na matawi zaidi ya elfu mbili mia tisa (2,900) nchini kote. Bofya hapa kutembelea tovuti yetu
Kuwa kizazi kinachotembea katika nguvu za Roho Mtakatifu na kuubadilisha ulimwengu kwa Neno la Mungu.
Kuwafikia wanafunzi wote kwa Injili ya Kristo kimkakati na kuwajenga kiroho kwa njia ya Kuabudu, Ushirika, Kufuasa ili waweze kuwahudumia watu wote kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Kuwafundisha wanafunzi kuyaishi maadili ya kikristo, kupiga vita matendo yote yanayoharibu jamii kama vile; Magonjwa ya zinaa, UKIMWI, Utoaji mimba, Ulevi, Utumiaji madawa ya kulevya, Ushoga, Usagaji, Ubakaji, pamoja na matendo mengine yote maovu.
Askofu mkuu wa TAG mnamo tarehe 28 mwezi wa pili aliapishwa Rasmi na kua Mwenyekiti wa CPCT.
Semina za ILI zinatarajiwa kuanza hivi karibuni hivyo basi viongozi na wanachama wote wanaotakiwa kuhudhulia msipange kukosa.
Kwenye semina za uongozi za ili kutakua na Mafunzo pia kuhusu Mfumo wetu wa Bezaleli hivyo basi Kamati za Sehemu, Kamati za Idara Sehemu na Jimbo mnahimizwa kuhudhulia.
soma zaidiKutakua na Semina ya Uongozi ya ILI zitakazofanyika CCT, Morogoro hivyo basi Waalimu wa Vyuo Mama na Wenza Wao wanahimizwa kufika bila kukosa.
soma zaidiKutakua na kikao cha tathmini ya robo ya I ya mwaka kitakachofanyika Morogoro na wahusika wakuu ni Kamati ya Utendaji /Menejimenti
soma zaidi