Miaka kumi na tatu ya Moto wa uamsho tunamtaka Bwana na nguvu zake






Ijue Idara ya Vijana

Jina la Idara ni Tanzania Assemblies of God - Christ's Ambassadors (CA's); Yaani ikiwa na maana ya Vijana mabalozi wa Kristo.'Kimsingi ni Idara ya Vijana'.

cas logo

MAONO

Maono ya Idara ya Vijana ni kua na Vijana:-

  • 1: Walio jaa Roho mtakatifu kikamilifu.
  • 2: Walio hamasika kihuduma.
  • 3: Wenye mzigo na uwezo wa kuvuna roho zilizopotea kwa ufanisi mkubwa.
  • 4: Kua na viongozi waaminifu na wawajibikaji katika ngazi zote.

DHIMA

idara ya Vijana wajumbe wa Kristo kwaajili ya: -

  1. Kuhamasisha vijana.
  2. Kuunganisha Vijana.
  3. Kulea vijana katika malezi bora.
  4. Kupandikiza vijana Mzigo na Maono ya; -
    • 1: Kuabudu kwa hiari yao baada ya kufundishwa umuhimu wa kumuabudu MUNGU.
    • 2: Kutumika kwa bidii na viwango vya juu.

MAKUSUDI

Makusudi ya Idara ni:-

  1. Kushuhudia.
    • Idara inawaandaa vijana kwa mafunzo mbalimbali na kuwahamasisha ili kwa kutumia mbinu na njia mbalimbali waweze kufanya uinjilisti wenye Nguvu utawawezesha kuwaleta watu wenyedhambi kwa Yesu.