
Rev. Dkt. Emmanuel Lazaro
Alikuwa Askofu Mkuu kuanzia mwaka 1967 mpaka 1998
Bofya ili kusoma
Maono yetu kama kanisa ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, kitaifa na kimataifa wakibatizwa katika Roho Mtakatifu huku tukiwa na ibada za kiroho, mafundisho halisi na sahihi ya Neno la Mungu na hivyo kuongezeka makanisa.
Bofya ili kusoma
Tanzania Assemblies of God (TAG) ipo kwa ajili ya kumuabudu Mungu katika Roho na kweli, katika kuuambia ulimwengu juu ya habari za Yesu na kuwapeleka waamini katika kumjua zaidi Yesu kupitia sifa, kuabudu na neno chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.
Bofya ili kusoma
Uaminifu Kibiblia, Uadilifu, Kuwajibika kijamii, Ushirikiano kama timu, Uvunaji kimkakati, Uwezeshaji wa uongoziUkuhani kwa waumini wote, Uwajibikaji wa usimamizi wa fedha, Ukuaji kimkakati, na Ubora.
Nembo ya kanisa itakuwa na muundo unaokaribia kufanana na ule wa makanisa mengi ya Assemblies of God duniani kote. Nembo hii itakuwa na maneno yanayosomeka “TANZANIA ASSEMBLIES OF GOD”, TAG, mchoro wa msalaba na Biblia, pamoja na mchoro mwingine mdogo wa Biblia wenye alama za mwale wa moto na njiwa, pamoja na maandishi “ALL THE GOSPEL”. Nembo ya kanisa pamoja na nembo ambazo zimewahi kutumiwa na TAG hapo awali zitasajiliwa chini ya Sheria ya Alama za Biashara na Huduma ya mwaka 1986.
Bendera ya kanisa itakuwa ya rangi ya bluu bahari na yenye nembo ya kanisa pamoja na maneno “JEHOVAH-NISSI”, yenye maana ya “BWANA ni Bendera yangu”. Bendera hii itakuwa sehemu ya utambulisho rasmi wa kanisa na taasisi zake popote pale, ndani na nje ya nchi.
Tanzania Assemblies of God (TAG) ilisajiliwa tarehe 21/10/1981 chini ya sheria ya Societies Ordinance ya mwaka 1954 na kupewa namba ya usajili SO. 6246.
Tanzania Assemblies of God ni kanisa lililotokana na uamsho mkubwa ulioanza huko mtaa wa Azusa, California nchini Marekani, mwanzoni mwa karne ya 20. Paul Deer ambaye awali alikuja kama mmishonari wa kujitegemea, na alianzisha Kanisa la Pentecoste Holiness Association (PHA) mnamo mwaka 1928 ambapo ibada ya kwanza hasa ya Kanisa hilo ilianza mapema mwaka 1929 huko Igale katika Wilaya ya Mbalizi mkoani Mbeya. Mnamo mwaka 1938 Derr alirejea Marekani na mwaka uliofuata 1939 alijiunga na Kanisa la Assemblies of God, na hivyo kuikabidhi kazi iliyokuwa imeanzishwa Tanzania (wakati huo ikiitwa Tanganyika) mikononi mwa Genenral Council ya Assemblies of God Marekani. Na kuuomba uongozi huo wampeleke Mmissionari kwenye kazi hiyo kuilea wakati yeye akiwa likizoni.
Historia inatuonesha kuwa katika miaka ya mwanzo kanisa lilisimamiwa na wamishonari wa kimarekani pamoja na wachungaji wa kiafrika wakati huo {Yohana Mpayo [Marehemu] na Petros) waliokuwa maaskofu chini ya Assemblies of God Mission. Kanisa liliendelea kuongozwa katika mfumo huo hadi mwaka 1967. Kanisa la kwanza kabisa la TAG lilikuwapo pale Igale wilaya ya Mbalizi mkoani Mbeya.Ni mwaka huo wa 1967, uongozi wa Assemblies of God Mission, uliamua kulikabidhi kanisa kwa uongozi wa wenyeji na Mchungaji Immanuel Lazaro, alichaguliwa kuwa Askofu Mkuu wa kwanza mtanzania wa kuongza Tanzania Assemblies of God (TAG) Kanisa hili liiingia hapa nchini kama matokeo ya uamsho mkubwa wa Kipentekoste uliotokea kule Azuza Marekani. Hivyo lengo kuu la kuanzishwa kwa kanisa ni kuwafikia wenye dhambi kwa injili iliyo hai, iletayo wokovu na kuleta uamsho mkubwa wa Bwana wetu Yesu Kristo hapa nchini. ili kutimiza lengo hilo ilikuwa lazima watendakazi shambani mwa Bwana waandaliwe tangu utoto.
Historia ya Maaskofu Wakuu wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God
Alikuwa Askofu Mkuu kuanzia mwaka 1967 mpaka 1998
Alikuwa Askofu Mkuu kuanzia mwaka 1992 mpaka 2008
Alianza kuwa Askofu mkuu mwaka 2008 hadi sasa
Tunaamini kwa dhati kuwa Biblia ndio Mwongozo wa imani yetu na matendo katika maisha yetu ya Kikristo. Tamko hili ndilo msingi wa ushirika wetu (1Kor.1:10; Mdo.2:42). Ukiri wa Imani yetu umejengwa katika misingi kumi na sita (16) ifuatayo:
Tunaamni kwamba Maandiko yote ya Agano la kale na yale ya Agano Jipya yamevuviwa kihalisi na MUNGU na ni Ufunuowa MUNGU kwa wanadamu, ni mamlaka ya mwisho ya imani (2Tim 3:15-17, 1The 2:13, 2Pet 1:2).
Tunaamini kwamba MUNGU mmoja tu aliye hai na wa kweli ambae amekwisha kujunua mwenyewe kama 'MIMI NIKO' wa milele, muumbaji wa Mbingu na nchi na na mkombozi wa ulimwengu na wanadmu.(kumb 6:4, Isa 43:20-11).
Tunaamini kwamba Bwana Yesu Kristo ni mwana wa MUNGU na anasifa zote za uungu (Yoh 1:1, lk 1:31-35, Mt 1:23).
Tunaamini kwamba Mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa MUNGU akiwa mzuri na mwema maana MUN GU alisema 'Na tumfanye mtu kwa mfano wetu na sura yetu' hata hivyo Mwanadamu kwa uasi wa hiari yake mwenyewe alianguka na kwa njia hiyo akajiletea mauti suo ya kimwili tu bali hata ya kiroho ambayo ni kutengwa mbali na MUNGU (Mwa 1:26-27; 2:17).
Tunaamini kua tumaini pekee la ukombozi wa Mwanadamu ni kwa njia ya damu ya Yesu Kristo Mwana wa MUNGU iliyomwagika.(Luk 24:47 yohana 3:3).
Tunaamini juu ya agizo la ubatizo wa kuzamisha linalotolewa na maandiko (Mt 28:19, Rum 6:4) Pia tunaamini juu ya meza ya Bwana mbayo ina mkate na matunda ya zabibu ni mfano wa kuelezea ushirika wetu wa asili ya Ki-MUNGU (2pet 1:4, 1Kor 11:26).
Tunaamini kwamba waamini wote wanatakiwa na wanahaki ya kutafuta ahadi ya Baba yaani ubatizo wa Roho Mtakatifu (Luk 26:46, 1Kor 12:1-36).
Tunaamini kwamba ubatizo wa waamini katika Roho Mtakatifu unashuhudiwa kwa ishara ya nje iliyo ya Kimwili ya kunena kwa lugha nyingine kwa Roho wa Mungu anavyowajalia (1Kor 12:4-10, 28).
Tunaamini kua utakaso ni tendo la kutengwa na kile kilicho kiovu na kujiweka wakfu kwaajili ya MUNGU (Rum 12:1-2, Ebr 13:12).
Tunaamini kwamba kanisa ni Mwili wa Kristo, Makao ya MUNGU kwa njia ya Roho, lenye vyeo vya Ki-MUNGU kwa ajili ya utimizo Kazi yake kuu (Efe 1:22-23, 2:22. Ebr 12:23).
Tunaamini kwamba huduma ya ki-Mungu pamoja na utumishi uliopangwa na maandiko umetolewa na Bwana wetu kwa makusudi matano: (Mk 16:15, Efe.4:11-13, Yh.4:23-24, 1Kor.12; Rum.12, Mdo.2:42-46).
Tunaamini kwamba uponyaji wa kimungu ni sehemu muhimu ya Injili. Kufunguliwa kutoka magonjwa na vifungo mbalimbali ni haki ya kila anayeamini (Isa. 53:4; 5;Mt.: 8:16;17; Yak. 5:14-16).
Tunaamini juu ya ufufuo wa wale ambao wamelala katika Kristo na kunyakuliwa kwao pamoja na wale waliohai waliosalia mpaka wakati wa kuja kwake Bwana ndilo tumaini lenye baraka na lililo kuu la Kanisa (1Thes.4:16, 17; Rum. 8:23; Tito 2:13; 1Kor.15:51, 52).
Tunaamini kuja kwa mara ya pili kwa Kristo ni pamoja na kunyakuliwa kwa Watakatifu ambalo ni tumaini lenye baraka, kukifuatiwa na kurudi kwa wazi kwa Kristo pamoja na Watakatifu wake kwa ajili ya kutawala hapa Ulimwenguni kwa muda wa miaka elfu moja (Zek. 14:5; Mt. 24:27;30; Ufu.1:7; 19;11-14; 20:1-6).
Tunaamini kwamba kutakuwepo na hukumu ya mwisho ambayo humo wafu waovu watafufuliwa na kuhukumiwa sawa sawa na matendo yao. Yeyote ambaye hatakutwa ameandikwa katika Kitabu cha Uzima, pamoja na Shetani na malaika zake, mnyama na nabii wa uongo, watatupwa katika adhabu ya milele katika ziwa liwakalo moto na kibiriti, ambayo ni mauti ya pili (Mt. 25:46; Mk.9:43-48; Ufu. 19:20;20:11-15; 21:8).
Kulingana na ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya ambamo haki yakaa ndani yake (2Pet.3:13; Ufu. 21 na 22).
Kwa maelezo zaidi Nunua katiba yetu sasa, Ili kununua
Uamsho ni Ajenda yetu.
Saa ya Uamsho ni Sasa.