Tunaamini katika Utatu Mtakatifu yaani Mungu Baba Mungu Mwana Mungu Roho Mtakatifu







MAONO

Bofya ili kusoma

Maono yetu kama kanisa ni kuwafanya watu kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo, kitaifa na kimataifa wakibatizwa katika Roho Mtakatifu huku tukiwa na ibada za kiroho, mafundisho halisi na sahihi ya Neno la Mungu na hivyo kuongezeka makanisa.

DHIMA

Bofya ili kusoma

Tanzania Assemblies of God (TAG) ipo kwa ajili ya kumuabudu Mungu katika Roho na kweli, katika kuuambia ulimwengu juu ya habari za Yesu na kuwapeleka waamini katika kumjua zaidi Yesu kupitia sifa, kuabudu na neno chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu.

MAADILI

Bofya ili kusoma

Uaminifu Kibiblia, Uadilifu, Kuwajibika kijamii, Ushirikiano kama timu, Uvunaji kimkakati, Uwezeshaji wa uongoziUkuhani kwa waumini wote, Uwajibikaji wa usimamizi wa fedha, Ukuaji kimkakati, na Ubora.

Nembo ya Kanisa

Nembo ya kanisa itakuwa na muundo unaokaribia kufanana na ule wa makanisa mengi ya Assemblies of God duniani kote. Nembo hii itakuwa na maneno yanayosomeka “TANZANIA ASSEMBLIES OF GOD”, TAG, mchoro wa msalaba na Biblia, pamoja na mchoro mwingine mdogo wa Biblia wenye alama za mwale wa moto na njiwa, pamoja na maandishi “ALL THE GOSPEL”. Nembo ya kanisa pamoja na nembo ambazo zimewahi kutumiwa na TAG hapo awali zitasajiliwa chini ya Sheria ya Alama za Biashara na Huduma ya mwaka 1986.